Skip to main content

Posts

Showing posts from 2011

KUMBU KUMBU ZA MWANA HAWA

MTUNZI: Odhiambo Danyell Manyunyu mepesi ya mvua yangesikika yakikung’uta mabati na kuibua mdundo flani iliozidisha tamaa yangu ya  kuendelea kupanga mbavu kwenye kitanda. Mara, alisikika jogoo mmoja kijijini akiwika kama kuashiria nuru ilikuwa imekubali zamu yake ya mchana. Nilibaki kugaragara kitandani huku mabishano makali yakiendelea akilini kati ya mwili dhaifu na nafsi yangu. Mwili ilisisitiza niendelee kulala huku nafsi ikinisihi niamke. Baada ya kutafakari kuhusu hasara za usingizi niliridhia kuamka. Ghafla, fikra zangu zilielekezwa katika saa kubwa iliyoning'inia ukutani ambayo ilikatiza hali ya unyamafu uliokuwa umetawala chumbani. kuzidisha, chenene fulani aliyekuwa kajificha mvunguni alianza kutoa sauti ya kuudhi. “Aah! Heri tuu niamke” nilijisemeza huku nikijikokota kuelekea kwenye dirisha. Nikichungulia nje, ningeona kunguru wakipigania makombo ya chakula kwenye pipa iliyosimama mkabala na chumba changu. Isitoshe, rukwama kukuu za wazegaz...

FEDHEHA ZA SWALEH

MTUNZI: MARIA REHEMA Swaleh kijana wa miaka ishirini na tisa alienda usingizini, akiwaza na kuwazua jinsi atakavyo jishindia jiko. Alihesabu miaka yake na kustaajabu kuwa miaka hiyo yote, alikuwa anavunda upweke. Kisa na maana hakuwa na bila barafu wa roho. Liwike lisiwike kutakucha. Swaleh aliamka na kabla ya kupata staftahi, alianza siku kwa kujipodoa. Liche ya uzito wake na kipipa cha tumbo, aliamua kuvaa shati na suruale iliyombana kupindukia. “ Ndo mavazi ya kisasa haya, nitaweza kuwapata warembo kadhaa,” alijiambia Swaleh. Baada ya staftahi, Swaleh huyo kiguu na njia jijini kutafuta kipenzi cha roho. Bak bandika bak bandua mpaka kwenye kituo cha basi. Alipoingia kwenye ‘matatu’ moja akakutana na kidosho aliyerembeka mno. Hakupoteza wakati alikimbia na kuketi karibu na mrembo huyo. Alivutiwa na macho yake makubwa yaliyong’aa na ngozi yake nyororo. Mwili wake je? Nikisema zaidi utamwonea wivu. Maumbile haya yalimtia Swaleh wazimu. Bila shaka Swaleh alibaki md...

NIMESADIKI MOMBASA NI KITOVU CHA STAREHE.

Na Odhiambo Danyell Mawingu mepesi yalitawanyika angani utadhani yameanikwa ili kukaushwa na miale ya jua ambayo yalikuwa yanazidi kufifia. Ghafla ,upepo mkali ulifagilia kwenye nchi kavu na kuwacha matawi ya miti yakipukutika ovyo ovyo kabla ya kuchezeshwa angani. Isitoshe, ilihamisha wingu moja baada ya nyingine hata anga ikabaki safi. Kilichobaki kuonekana ni kundi ndogo la kunguru

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

KULIFANYIKA NINI KATIKA KONGAMANO LA AFYA NA MAENDELEO - SAFARI PARK

“Aisee! nani anashukia safari park?” Makanga wa matatu ya kuelekea Githurai alipaza sauti akiuliza. “Mimi hapa!” nilimjibu huku nikikazana kupenya katikati ya abiria. Hewani, palishiba midundo mizito ya mziki iliyosambazwa kupitia spika kubwa zilizostiriwa chini ya viti. “Hujaniregeshea change yangu!” nilimkabili makanga mlangoni. “Ulinipa pesa ngapi?” aliuliza akihema utadhani ni yeye amebeba gari kutoka mjini. Kuvutia zaidi, kijasho chembamba kilimtiririka njia mbili mbili mashavuni na kudondoka kwenye shati yake ya manjano. Kwa sekunde chache, nilizubaishwa na mavazi ya makanga yule wa kiwiliwili cha wastani. Kichwani alivalia kofia nyekundu ya kuchujuka rangi iliyonakshiwa na maandishi “kazi kwa vijana”.Kiwiliwili kilijificha ndani ya kabuti kubwa iliyomfanya afanane "hatari bin danger" Mashavuni palisongamana “msitu” ndevu zilizochakaa hata nikashuku ni makao wanyama pori. Taya (jaws) zake nazo zilichapa kazi ungedhani ni mtambo wa kusaga mahindi. Gololi za macho ...

BIBI WA KUTAFUTIWA!

Kwa Bi Saida S.L.P 248 DAYSTAR, Athi-River 24/03/2011 Mama, Habari za siku nyingi? Hivi naamini u salama wasalmin hata ikiwa utasema nmenyamaza sana. Kabla sijaendelea, ningependa kuuliza ikiwa ulipata gora ya leso niliyokutumia. Hata hivyo,Kama ulipata ni sawa. Mama! Lengo na madhumuni ya kuiandika barua hii ni kulalama kuhusu binti mliyenitafutia. Naamini nyina hawezi kumpa mwanawe sumu. Lakini, ni wazi tunda ulilonichagulia kumbe ilivutia kwa nje ilhali ndani imeoza. Sitaki nikupandishe presha bure, lakini, ni vema nikufichulie dosari zake kabla maji hayajazidi unga. Mama! Kitanda cha kifahari nimenunua lakini amini usiamini nimelala kila kukicha nikijishika tama. Kisa na maana, bibi ni mwana riadha wa usiku. Kabla nifikie kuiandika barua hii. Nimetafuta ushauri kutoka kwa wataalamu wa kila aina. Lakini, tiba imeshindikana. Nimechoka kulipa dhamana ya kumkomboa kila anapotiwa nguvuni na askari wa baraza la jiji kwa shtaka la kukimbia ovyo usiku. Hivi nikizungumza, tay...

SIRI ZA CHUO KIKUU CHA DAYSTAR

Njoo unisome kwa makini S.L.P 927 MACHO PLAZA Kwa wewe unayenisoma, Habari za utokako? Naona unahema kweli ukitaka kujua yaliyojiri hivi leo kwenye barua hii. Hee! By the way, ikiwa wataka tuelewane naomba uwache kuniangalia kwa hizo macho za kushiba chuki na dharau. Kabla nikuendelezee udaku! Tafadhali wacha kuangalia kando kando ukinisoma. Unawafanya wapita njia wanadhani tunawasengenya humu. By the way, usha ambiwa na yeyote hivi leo kwamba watamanisha? Ooooooooooooh! Nisamehe. I mean.... you are fearfully and wonderfully made. Sitaongeza wala sitapunguza. Niwie radhi siwes kutranslate, please! Mwelezee.. aliye kando yako aje akusaidie. Kabla nikupatie udaku, natamani niulize swali moja tuu. Nihakikishie kwamba hutanuna! Naogopa lakini heri niulize tuu atleast tusafiane nia. Hivi mbona una blush sana? Kama nimekubamba si uniambie tuu ama uwaite wanafunzi wenzako waje wasome uhondo. Matawi ya miti naona inapukutika kutokana na upepo mkali unaofagilia kutoka milima ya l...

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU “SEASON TWO”

“Darling funga macho nikuambie kitu” Bahati alinishurutisha kwa sauti ya upole. Bila kusita, nilifikicha macho yangu kwa viganja vya mkono nikiwa na hamu ya kujua kilichokuwa chaningoja. Bahati alikuwa na uzoefu wa kunifanyia utani wa aina hii haswa wakati penzi lilkuwa limemchachawiza. Mara ya mwisho alitumia mbinu hii, ni wakati aliponiletea pete ya dhahabu afisini. Wakati nilipokuwa nimeziba macho, mawazo mengi yaligongana akilini. “labda ana siri Fulani anataka kunieleza ama ni zawadi anataka kunipa? aaah! Potelea mbali, liwe liwalo!” nilijisemeza moyoni. Ghafla, Mlipuko mkubwa ulisikika hatua chache. sekunde kadhaa baadaye, nilijipata nimelala kifudifudi ardhini huku shati yangu ikitoja damu. “Mungu wangu! Mungu wangu! ” nilibaki kupiga kite huku nikichirizikwa ovyo na damu utosini. Nilikazana kulinda nguvu kiasi niliyokuwa nimebaki nayo, macho yangu yalipepesa na kuranda randa ovyo nikitafuta alipokuwa Bahati wangu. Mita chache, niliona mawimbi ya bahari yenye hasira y...

KUAGA KWA GWIJI, MJ

Dunia iliomboleza, kulala kwa Gwiji MJ tulimpoteza, vilio kwenye miji Mauti umetukaza, Na tukutane kwa jaji Kwaheri ya kuonana Mfalme wa Pop Mauti huna arafa, tutayarishe mapema Robot densi ilifaa, moon walk ikavuma Ingawa ulikufa, sifa zitakusakama Kwaheri ya kuonana Mfalme wa Pop Mahasidi wenye wivu, kakupeleka kizimba Wakakupa maumivu, bila hatia ukaimba Umerudi kuwa jivu, kwetu ungali simba Kwaheri ya kuonana Mfalme wa Pop Mahala pema peponi, Na ilale roho yako Takulinda kama mboni, zisipotee sifa zako Sinayo woga usoni, kukupea wewe heko Kwaheri ya kuonana Mfalme wa Pop

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta. Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho. Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni . Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo. “Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa...

Kwa mpenzi wangu Bi Omena.

Rashidy Mpendwa Kwa mpenzi wangu Bi Omena. Sanduku la posta 10, Jangwani. Lazizi, Mwaaaaah! ama wataka busu nyingine? Nimeandika barua hii kwa hofu kuu kwani naogopa hii ni mara ya mwisho tutakutana kwenye mji mkuu wa sahani. Amini usiamini, nitamisi sana tabia yako nzuri ya kunitengezea kitoweo cha kufinyanga kwa sima wa mahindi. Kwa hakika, sina furaha kwani ahadi zako kwamba tutakutana sokoni zimeambulia patupu.kila wakati nimeenda sokoni sijakupata. nimewapata tuu mandugu na madada zako kiboma, kambare, mbuta na tilapia. Shemeji yako Tilapia ameniarifu kwamba idadi ya familia yenu imepungua sana katika ziwa victoria. Kisa na maana,Tilapia aliteta vikali kwamba chemichemi ya maji ya mau imeharibiwa pakubwa na jamii ya wanadamu. ailisistiza kwamba msitu huo uhifadhiwe ikiwa nataka kuonja tena kitoweo chako. Mpenzi, wajua kwamba nakuota kila nikila? matonge ya sima yananinyonga kila nikiwaza kukuhusu. By the way nimeamua nitakujengea bonge la swimming pool uje uishi na fam...