Skip to main content

SIRI ZA CHUO KIKUU CHA DAYSTAR

Njoo unisome kwa makini
S.L.P 927
MACHO PLAZA
Kwa wewe unayenisoma,

Habari za utokako? Naona unahema kweli ukitaka kujua yaliyojiri hivi leo kwenye barua hii. Hee! By the way, ikiwa wataka tuelewane naomba uwache kuniangalia kwa hizo macho za kushiba chuki na dharau.

Kabla nikuendelezee udaku! Tafadhali wacha kuangalia kando kando ukinisoma. Unawafanya wapita njia wanadhani tunawasengenya humu. By the way, usha ambiwa na yeyote hivi leo kwamba watamanisha? Ooooooooooooh! Nisamehe. I mean.... you are fearfully and wonderfully made. Sitaongeza wala sitapunguza.

Niwie radhi siwes kutranslate, please! Mwelezee.. aliye kando yako aje akusaidie.
Kabla nikupatie udaku, natamani niulize swali moja tuu. Nihakikishie kwamba hutanuna! Naogopa lakini heri niulize tuu atleast tusafiane nia. Hivi mbona una blush sana? Kama nimekubamba si uniambie tuu ama uwaite wanafunzi wenzako waje wasome uhondo.

Matawi ya miti naona inapukutika kutokana na upepo mkali unaofagilia kutoka milima ya lukenya. Woishe nishikilie! Naogopa itanipeperusha na huenda nikatua penye maadui wa lugha tamu ya Kiswahili.

Back to business! Nina aibu kubwa kukutangazia habari hii. Aaah! Woga potelea mbali. Je! Umesikia kwamba? hivi majuzi wakora wamevamia hoteli moja kule off kampus na kuiba mali inayokisiwa kuwa ya takriban shilingi elfu tano. Hii inajumlisha vipande kadha za ugali wembe pamoja na sufuria ya “nyama”

Duru za kuaminika zilieleza ukurasa huu kwamba CCTV kamera iliyowekwa kwenye hoteli hiyo ya mabati iliwanasa wakora hao wakitekeleza maovu yao. Majina yashatambuliwa ila sitaki kueneza uvumi. Usimwambie mtu lakini nimewasikia watu wakisema genge hilo sugu lilikuwa kwenye orodha maarufu ya “OCAMPO 600”

Kulingana na mwenye hoteli hiyo, genge hilo lilijitokeza likiwa limejiami na bunduki bandia kabla ya kuamrisha wateja kulala chini. Baadaye walifanikiwa kukutoroka na sufuria moja ambayo walidhani ni ya nyama kumbe ilikuwa yenye maji ya kuosha vyombo pamoja na vipande hivyo vya ugali.

Nishakwambia! Ndo maana nikapewa jina barua na jukumu langu likawa ni kusafirisha ujumbe.

Kumbuka kunisoma kila ijumaa nkupe yaliyojiri katika ulimwengu wa umbea. kuwasiliana nami mtumie bosi wangu ujumbe kupitia kujiuunga na kundi la WAKIDA kwenye mtandao wa FACEBOOK ama msikize kila alhamisi jioni kwenye idhaa ya SHINE FM 103.1 katika kipindi cha KIMBUNGA CHA JIONI.

akhsante kwa wakati wako,

niite Odhiambo Danyell ama ukipenda Rashidy

nimeondoka.....

Comments

my say my take said…
maneno mazuri haya nataajia kuona mengi
tasha said…
i like baby........
nawashkuru warembo kwa kuendelea kutembelea ukurasa huu!

Popular posts from this blog

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta. Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho. Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni . Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo. “Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa...

SIRI ZA “JAM” JIJINI NAIROBI; TOLEO LA PILI

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Jinsi basi lilivyozidi kufukuzia kuelekea mzunguko wa Nyayo stadium, ndivyo ilizidi kuwachilia moshi ya mpingo iliyosokota angani kabla ya kutawanyika. Pale pia, tulimpata polisi wa trafiki mwanamke aliyefungia mshipi wa longi yake kwenye kifua. Amini usiamini, kwa ishara ya mkono alielekeza mkondo wa gari kama jinsi upepo huele ... keza bendera. Pale tulis...imama kwa dakika chache kabla ya msongamano kufunguliwa. Cha kuvutia tamaa ya macho yangu ilikuwa ‘tuk tuk’ fulani ambayo ilipenya penya kati kati ya magari huku ikipiga kelele kama mashine ya kusaga mahindi. Wenzangu wanaiita kule bara POSHOMILL. “We! Boss, ondoa hiyo kabati kwenye barabara” alisikika akishambuliwa na mmoja wa madereva wa matatu. Wanasema muungwana hununa moyoni na wala siyo mashavuni na kwa hivyo Yule dereva wa ‘tuk tuk’ akaridhia kumjibu kwa kimya. Kando na tukio hili, kuna jambo lililotendeka ambalo liliwacha mbavu za kila mtu zikiuma. Niseme nisiseme! Aaaah! ...