Njoo unisome kwa makini
S.L.P 927
MACHO PLAZA
Kwa wewe unayenisoma,
Habari za utokako? Naona unahema kweli ukitaka kujua yaliyojiri hivi leo kwenye barua hii. Hee! By the way, ikiwa wataka tuelewane naomba uwache kuniangalia kwa hizo macho za kushiba chuki na dharau.
Kabla nikuendelezee udaku! Tafadhali wacha kuangalia kando kando ukinisoma. Unawafanya wapita njia wanadhani tunawasengenya humu. By the way, usha ambiwa na yeyote hivi leo kwamba watamanisha? Ooooooooooooh! Nisamehe. I mean.... you are fearfully and wonderfully made. Sitaongeza wala sitapunguza.
Niwie radhi siwes kutranslate, please! Mwelezee.. aliye kando yako aje akusaidie.
Kabla nikupatie udaku, natamani niulize swali moja tuu. Nihakikishie kwamba hutanuna! Naogopa lakini heri niulize tuu atleast tusafiane nia. Hivi mbona una blush sana? Kama nimekubamba si uniambie tuu ama uwaite wanafunzi wenzako waje wasome uhondo.
Matawi ya miti naona inapukutika kutokana na upepo mkali unaofagilia kutoka milima ya lukenya. Woishe nishikilie! Naogopa itanipeperusha na huenda nikatua penye maadui wa lugha tamu ya Kiswahili.
Back to business! Nina aibu kubwa kukutangazia habari hii. Aaah! Woga potelea mbali. Je! Umesikia kwamba? hivi majuzi wakora wamevamia hoteli moja kule off kampus na kuiba mali inayokisiwa kuwa ya takriban shilingi elfu tano. Hii inajumlisha vipande kadha za ugali wembe pamoja na sufuria ya “nyama”
Duru za kuaminika zilieleza ukurasa huu kwamba CCTV kamera iliyowekwa kwenye hoteli hiyo ya mabati iliwanasa wakora hao wakitekeleza maovu yao. Majina yashatambuliwa ila sitaki kueneza uvumi. Usimwambie mtu lakini nimewasikia watu wakisema genge hilo sugu lilikuwa kwenye orodha maarufu ya “OCAMPO 600”
Kulingana na mwenye hoteli hiyo, genge hilo lilijitokeza likiwa limejiami na bunduki bandia kabla ya kuamrisha wateja kulala chini. Baadaye walifanikiwa kukutoroka na sufuria moja ambayo walidhani ni ya nyama kumbe ilikuwa yenye maji ya kuosha vyombo pamoja na vipande hivyo vya ugali.
Nishakwambia! Ndo maana nikapewa jina barua na jukumu langu likawa ni kusafirisha ujumbe.
Kumbuka kunisoma kila ijumaa nkupe yaliyojiri katika ulimwengu wa umbea. kuwasiliana nami mtumie bosi wangu ujumbe kupitia kujiuunga na kundi la WAKIDA kwenye mtandao wa FACEBOOK ama msikize kila alhamisi jioni kwenye idhaa ya SHINE FM 103.1 katika kipindi cha KIMBUNGA CHA JIONI.
akhsante kwa wakati wako,
niite Odhiambo Danyell ama ukipenda Rashidy
nimeondoka.....
S.L.P 927
MACHO PLAZA
Kwa wewe unayenisoma,
Habari za utokako? Naona unahema kweli ukitaka kujua yaliyojiri hivi leo kwenye barua hii. Hee! By the way, ikiwa wataka tuelewane naomba uwache kuniangalia kwa hizo macho za kushiba chuki na dharau.
Kabla nikuendelezee udaku! Tafadhali wacha kuangalia kando kando ukinisoma. Unawafanya wapita njia wanadhani tunawasengenya humu. By the way, usha ambiwa na yeyote hivi leo kwamba watamanisha? Ooooooooooooh! Nisamehe. I mean.... you are fearfully and wonderfully made. Sitaongeza wala sitapunguza.
Niwie radhi siwes kutranslate, please! Mwelezee.. aliye kando yako aje akusaidie.
Kabla nikupatie udaku, natamani niulize swali moja tuu. Nihakikishie kwamba hutanuna! Naogopa lakini heri niulize tuu atleast tusafiane nia. Hivi mbona una blush sana? Kama nimekubamba si uniambie tuu ama uwaite wanafunzi wenzako waje wasome uhondo.
Matawi ya miti naona inapukutika kutokana na upepo mkali unaofagilia kutoka milima ya lukenya. Woishe nishikilie! Naogopa itanipeperusha na huenda nikatua penye maadui wa lugha tamu ya Kiswahili.
Back to business! Nina aibu kubwa kukutangazia habari hii. Aaah! Woga potelea mbali. Je! Umesikia kwamba? hivi majuzi wakora wamevamia hoteli moja kule off kampus na kuiba mali inayokisiwa kuwa ya takriban shilingi elfu tano. Hii inajumlisha vipande kadha za ugali wembe pamoja na sufuria ya “nyama”
Duru za kuaminika zilieleza ukurasa huu kwamba CCTV kamera iliyowekwa kwenye hoteli hiyo ya mabati iliwanasa wakora hao wakitekeleza maovu yao. Majina yashatambuliwa ila sitaki kueneza uvumi. Usimwambie mtu lakini nimewasikia watu wakisema genge hilo sugu lilikuwa kwenye orodha maarufu ya “OCAMPO 600”
Kulingana na mwenye hoteli hiyo, genge hilo lilijitokeza likiwa limejiami na bunduki bandia kabla ya kuamrisha wateja kulala chini. Baadaye walifanikiwa kukutoroka na sufuria moja ambayo walidhani ni ya nyama kumbe ilikuwa yenye maji ya kuosha vyombo pamoja na vipande hivyo vya ugali.
Nishakwambia! Ndo maana nikapewa jina barua na jukumu langu likawa ni kusafirisha ujumbe.
Kumbuka kunisoma kila ijumaa nkupe yaliyojiri katika ulimwengu wa umbea. kuwasiliana nami mtumie bosi wangu ujumbe kupitia kujiuunga na kundi la WAKIDA kwenye mtandao wa FACEBOOK ama msikize kila alhamisi jioni kwenye idhaa ya SHINE FM 103.1 katika kipindi cha KIMBUNGA CHA JIONI.
akhsante kwa wakati wako,
niite Odhiambo Danyell ama ukipenda Rashidy
nimeondoka.....
Comments