Skip to main content

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo

Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta.

Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili.

Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya.

Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi.

Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa.

Mahuluku taabu nawafananisha na mshale wa kuhesabia sekunde kwa maana, wao hufanya kazi zaidi hata ingawa maumbile yao yameshiba unyonge. Kama tuu mshale wa sekunde, wenyeji katika kiwango hiki hulazimishwa kulipa kodi hata ingawa kipato ni kilegevu.

Ukihesabu, utagundua kwamba mshale wa sekunde huzunguka mara elfu moja mianne na arobaini kila siku. Si bure, wakenya hawa huandamana kila mara kutokana na unyanyasaji unaofanywa dhidi yao.

Kwingineko, mshale wa kadri ama ukipenda wa kurekodi dakika unalingana na wakenya wa maisha ya wastani. Kiwango hiki chajumlisha wale walomudu kupata elimu na hatimaye wakabahatika kuhifadhi nafasi za katikati serikalini na katika kampuni za kibinafsi.

Hapa, kazi ni kiasi na kipato ni kiasi ndo maana mshale wa dakika huzunguka mara ishirini na nne pekee kwa siku . hebu tafakari tofauti kubwa iliyoko ikilingana na kazi ya mshale ya sekunde.

Mwishowe, kuna ile mshale wa kuhesabu masaa. Kimatani anaitwa “hatunganani ila twavuma” bwana huyu anasifika kwa unyanyasaji dhidi ya wenzake. Hata ingawa huzunguka mara mbili tuu kwa siku, yeye ndiye mwenye ushawishi zaidi.

Kimaumbile, yeye ni mfupi na kibonge. Isitoshe, itakubidi ukaze macho zaidi ili kumwona akitekeleza wajibu wake. Katika Kenya yetu, mshale huu unafananishwa na viongozi wetu ambao kazi yao imekua ni kupayuka na kutoa ahadi za uwongo huku wakizidi kufilisi mlipa kodi.

Hebu sasa tazama viwango tofauti katika jamii ukilinganisha na mishale hizi za saa. Kazi ya wanasiasa pamoja na wale wa kipato cha wastani kamwe haiwezi kulinganishwa na jasho ya wakenya wanaopata malipo ya chini ya dola kwa siku.

Jee! Itakuwaje siku moja mshale ya kuhesabu sekunde ikisusia kazi? Hata labda hii ndoo maana ya wewe kuchelewa kwenda darasani ama kazini leo asubuhi.

Comments

Unknown said…
Interesting perspective,,very interesting.

Popular posts from this blog

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta. Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho. Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni . Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo. “Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa...

SIRI ZA “JAM” JIJINI NAIROBI; TOLEO LA PILI

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Jinsi basi lilivyozidi kufukuzia kuelekea mzunguko wa Nyayo stadium, ndivyo ilizidi kuwachilia moshi ya mpingo iliyosokota angani kabla ya kutawanyika. Pale pia, tulimpata polisi wa trafiki mwanamke aliyefungia mshipi wa longi yake kwenye kifua. Amini usiamini, kwa ishara ya mkono alielekeza mkondo wa gari kama jinsi upepo huele ... keza bendera. Pale tulis...imama kwa dakika chache kabla ya msongamano kufunguliwa. Cha kuvutia tamaa ya macho yangu ilikuwa ‘tuk tuk’ fulani ambayo ilipenya penya kati kati ya magari huku ikipiga kelele kama mashine ya kusaga mahindi. Wenzangu wanaiita kule bara POSHOMILL. “We! Boss, ondoa hiyo kabati kwenye barabara” alisikika akishambuliwa na mmoja wa madereva wa matatu. Wanasema muungwana hununa moyoni na wala siyo mashavuni na kwa hivyo Yule dereva wa ‘tuk tuk’ akaridhia kumjibu kwa kimya. Kando na tukio hili, kuna jambo lililotendeka ambalo liliwacha mbavu za kila mtu zikiuma. Niseme nisiseme! Aaaah! ...