Kwa Bi Saida
S.L.P 248
DAYSTAR, Athi-River
24/03/2011
Mama,
Habari za siku nyingi? Hivi naamini u salama wasalmin hata ikiwa utasema nmenyamaza sana. Kabla sijaendelea, ningependa kuuliza ikiwa ulipata gora ya leso niliyokutumia. Hata hivyo,Kama ulipata ni sawa.
Mama! Lengo na madhumuni ya kuiandika barua hii ni kulalama kuhusu binti mliyenitafutia. Naamini nyina hawezi kumpa mwanawe sumu. Lakini, ni wazi tunda ulilonichagulia kumbe ilivutia kwa nje ilhali ndani imeoza.
Sitaki nikupandishe presha bure, lakini, ni vema nikufichulie dosari zake kabla maji hayajazidi unga. Mama! Kitanda cha kifahari nimenunua lakini amini usiamini nimelala kila kukicha nikijishika tama. Kisa na maana, bibi ni mwana riadha wa usiku.
Kabla nifikie kuiandika barua hii. Nimetafuta ushauri kutoka kwa wataalamu wa kila aina. Lakini, tiba imeshindikana. Nimechoka kulipa dhamana ya kumkomboa kila anapotiwa nguvuni na askari wa baraza la jiji kwa shtaka la kukimbia ovyo usiku.
Hivi nikizungumza, tayari nishamweka kwenye basi ya kurudi alikotoka. Heri nijichagulie bibi hata kam nitaenda kinyume na na itikadi zetu.
Najuta ni kwanini nikakubali kauli yenu ya kumfukuza mpenzi wangu njoki kwa madai kwamba ni wa kabila tofauti.
Mama! najua umeudhika kwa vile nimepinga kauli yenu. Kumbuka ulinieleza kwamba mwana akinyelea paja halikatwi bali hupanguswa.
Nitakuja nyumbani jumapili ijayo tupate kujadiliana zaidi.
Mimi Mwanao
Radhia Onyango
S.L.P 248
DAYSTAR, Athi-River
24/03/2011
Mama,
Habari za siku nyingi? Hivi naamini u salama wasalmin hata ikiwa utasema nmenyamaza sana. Kabla sijaendelea, ningependa kuuliza ikiwa ulipata gora ya leso niliyokutumia. Hata hivyo,Kama ulipata ni sawa.
Mama! Lengo na madhumuni ya kuiandika barua hii ni kulalama kuhusu binti mliyenitafutia. Naamini nyina hawezi kumpa mwanawe sumu. Lakini, ni wazi tunda ulilonichagulia kumbe ilivutia kwa nje ilhali ndani imeoza.
Sitaki nikupandishe presha bure, lakini, ni vema nikufichulie dosari zake kabla maji hayajazidi unga. Mama! Kitanda cha kifahari nimenunua lakini amini usiamini nimelala kila kukicha nikijishika tama. Kisa na maana, bibi ni mwana riadha wa usiku.
Kabla nifikie kuiandika barua hii. Nimetafuta ushauri kutoka kwa wataalamu wa kila aina. Lakini, tiba imeshindikana. Nimechoka kulipa dhamana ya kumkomboa kila anapotiwa nguvuni na askari wa baraza la jiji kwa shtaka la kukimbia ovyo usiku.
Hivi nikizungumza, tayari nishamweka kwenye basi ya kurudi alikotoka. Heri nijichagulie bibi hata kam nitaenda kinyume na na itikadi zetu.
Najuta ni kwanini nikakubali kauli yenu ya kumfukuza mpenzi wangu njoki kwa madai kwamba ni wa kabila tofauti.
Mama! najua umeudhika kwa vile nimepinga kauli yenu. Kumbuka ulinieleza kwamba mwana akinyelea paja halikatwi bali hupanguswa.
Nitakuja nyumbani jumapili ijayo tupate kujadiliana zaidi.
Mimi Mwanao
Radhia Onyango
Comments
thanks! thanks! thanks!