Skip to main content

BIBI WA KUTAFUTIWA!

Kwa Bi Saida
S.L.P 248
DAYSTAR, Athi-River
24/03/2011

Mama,
Habari za siku nyingi? Hivi naamini u salama wasalmin hata ikiwa utasema nmenyamaza sana. Kabla sijaendelea, ningependa kuuliza ikiwa ulipata gora ya leso niliyokutumia. Hata hivyo,Kama ulipata ni sawa.

Mama! Lengo na madhumuni ya kuiandika barua hii ni kulalama kuhusu binti mliyenitafutia. Naamini nyina hawezi kumpa mwanawe sumu. Lakini, ni wazi tunda ulilonichagulia kumbe ilivutia kwa nje ilhali ndani imeoza.

Sitaki nikupandishe presha bure, lakini, ni vema nikufichulie dosari zake kabla maji hayajazidi unga. Mama! Kitanda cha kifahari nimenunua lakini amini usiamini nimelala kila kukicha nikijishika tama. Kisa na maana, bibi ni mwana riadha wa usiku.

Kabla nifikie kuiandika barua hii. Nimetafuta ushauri kutoka kwa wataalamu wa kila aina. Lakini, tiba imeshindikana. Nimechoka kulipa dhamana ya kumkomboa kila anapotiwa nguvuni na askari wa baraza la jiji kwa shtaka la kukimbia ovyo usiku.

Hivi nikizungumza, tayari nishamweka kwenye basi ya kurudi alikotoka. Heri nijichagulie bibi hata kam nitaenda kinyume na na itikadi zetu.

Najuta ni kwanini nikakubali kauli yenu ya kumfukuza mpenzi wangu njoki kwa madai kwamba ni wa kabila tofauti.

Mama! najua umeudhika kwa vile nimepinga kauli yenu. Kumbuka ulinieleza kwamba mwana akinyelea paja halikatwi bali hupanguswa.

Nitakuja nyumbani jumapili ijayo tupate kujadiliana zaidi.

Mimi Mwanao
Radhia Onyango

Comments

nimo wa wambui said…
at first i thought mwanariadha wa usiku??????? wa wa hii iko juu
my say my take said…
nyc stuff keep it up i lyk it
@Nimo na Annabel shukran sana kwa mchango wenu katika ukurasa huu bila ya nyinyi hapa patakosa ladha. waalikeni wenzenu.

thanks! thanks! thanks!

Popular posts from this blog

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta. Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho. Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni . Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo. “Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa...

SIRI ZA “JAM” JIJINI NAIROBI; TOLEO LA PILI

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Jinsi basi lilivyozidi kufukuzia kuelekea mzunguko wa Nyayo stadium, ndivyo ilizidi kuwachilia moshi ya mpingo iliyosokota angani kabla ya kutawanyika. Pale pia, tulimpata polisi wa trafiki mwanamke aliyefungia mshipi wa longi yake kwenye kifua. Amini usiamini, kwa ishara ya mkono alielekeza mkondo wa gari kama jinsi upepo huele ... keza bendera. Pale tulis...imama kwa dakika chache kabla ya msongamano kufunguliwa. Cha kuvutia tamaa ya macho yangu ilikuwa ‘tuk tuk’ fulani ambayo ilipenya penya kati kati ya magari huku ikipiga kelele kama mashine ya kusaga mahindi. Wenzangu wanaiita kule bara POSHOMILL. “We! Boss, ondoa hiyo kabati kwenye barabara” alisikika akishambuliwa na mmoja wa madereva wa matatu. Wanasema muungwana hununa moyoni na wala siyo mashavuni na kwa hivyo Yule dereva wa ‘tuk tuk’ akaridhia kumjibu kwa kimya. Kando na tukio hili, kuna jambo lililotendeka ambalo liliwacha mbavu za kila mtu zikiuma. Niseme nisiseme! Aaaah! ...