MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL
SEHEMU YA KWANZA:
Endelea kufuatilia hadithi hii kujua kinachojiri!!!!!........
SEHEMU YA KWANZA:
Mzee Matendechere alionekana kuokotwa na usingizi mwepesi wakati akiuguza majeraha ya panga hospitalini. Kisa na maana, adabu ilimhama mkewe hata akaamua kuchukua sheria mkononi na kumpa mumewe kichapo cha mbwa kabla ya kutorokea kusichojulikana.
Kichwa chake kilibanwa kwa kilemba cheupe chenye matone ya damu. Isitoshe, Kwenye shavu la kushoto, palidhihirika jeraha bichi lenye kushonwa kwa uzi. Cha kusikitisha zaidi, Pembezoni mwa kitanda, wangeonekana wapiga picha kutoka vyumba vya habari waking’ang’ana kuchukua picha za kuvutia watazamaji.
picha kwa hisani ya http://medievalminds.com |
Maskini Matendechere alizidiwa na usingizi hata akabakia kukoroma huku akifungua mdomo mithili ya mamba mwenye njaa. “Wow! This seems to be the best shot, I,m loving this” alisikika akisema mmoja wa wapigaji picha tuliyeshuku ni wa asili ya kimarekani. Kweli, vita vya panzi furaha ya kunguru.
Wakati haya yakijiri, ndoto ya matukio yaliyotendeka kabla ya masaibu haya kumpata Matendechere yalivamia mawazo yake. Akilini, alijaribu kukusanya picha hizo bila ya kitendawili cha asili ya maumivu yake kuteguka.
Midundo mizito ya rumba ilizidi kufagilia katika mkahawa maarufu wa ‘tamasha’ katika barabara ya tugawe umaskini. Kama kuchokoza wenye kuneng’ua viuno kwenye sakafu, Deejay Manyoya aliwachilia kibao maarufu ‘I,m not sober’ cha bendi maarufu ya Jamnazi Afrika. Kauli hii ilisindikizwa na vifijo na nderemo. ungedhani ni karamu ya kukaribisha kurudi kwa Yesu. Haya yakijiri, baadhi ya wenyeji walizidi kumimina chupa za mvinyo macho wakibandika kwenye runinga.
Wakati huu wote, Mzee Matendechere alikuwa amechokorwa kichwa na mizimwi ya mvinyo kiasi ya kwamba aliridhia kutafuta starehe kwenye kochi kando ya ‘counter’.
Ukitizama kushoto, ungeona kundi la makahaba ambao walikuwa wamejikwatua kwatu kwatu wakianika mitego yao tayari kunasa wateja. Mwingine alivalia ‘tumbo cut’ ya kubana kifua yenye maandishi “usiseme maziwa, sema ngombe”. Isitoshe, alivalia sketi fupi iliyofichua mapaja yake yenye madoadoa utadhani ni wa jamii ya chui au fisi.
Wakati viumbe hawa wakisasambua mapaja yao kwa wapita njia, Mzee Matendechere alibakia kuvuta mabaki ya sigara yaliyoangushwa na wateja sakafuni. Baba mtu alizubaishwa na vimulimuli vya taa ya ‘disco light’ akakaribisha moshi ndani ya mapafu kabla ya kuwachilia wingu kubwa hewani.
“Mzee! Inuka uende nyumbani. Tuko karibu kufunga na hatutaki ukamatwe na polisi” wahudumu pale kwenye mkahawa walimrai. “Kwani huyo Mututho anadhani ni nani atupimie starehe na pesa tunakunywa ni zetu? Leta kingfisher mbili hapo.” alisikika Matendechere akizusha kwa ujeuri huku akilaani mbunge aliyebuni sheria inayopima masaa ya kunywa pombe.
Wakati Matendechere akizizana na wale wahudumu , ghafla fikra zake zilivutiwa na maandishi FulanI ukutani. “Customers have a right to stay and to pay”. “Haya ndiyo madhara ya kususia masomo mapema. Can you please read the bold writings on the wall?” Mzee Matendechere aliwakabili huku akionekana kuzidiwa na kichefuchefu.
Kwa dakika zile chache, baba mtu alijiona jogoo wa kukomaa. kuwika kwake kuliwatisha wahudumu. Kwenye lango kuu la mkahawa, tayari wateja wengine wangeonekana wakiondoka wameshikana taratibu kumaanisha walikuwa wameona dalili ya . Kadri masaa yalivyoyoma ndivyo shughuli zilipungua pale hata mziki ikazimwa na stima kuzimwa.
“Ala! Mzee, hii ni siku ya pili tunakutoa hapa kwa nguvu. Kwani huna familia? Enda nyumbani tunafunga.” Askari aliyeshika doria langoni alimzomea Matendechere.
Baadaye, baba mtu aliona amezidiwa maarifa hata akajikusanya na kutembea taratibu akieleka nyumbani. Barabarani, hungempita bila ya kumtambua kutokana na kuimba kwake. “I,m not sober Odiero, I,m not sober……..i,m not sober because I,ve taken guiness.”hivyo ndivyo hali ilikuwa.
Ilibakia kona moja tuu kabla ya kuwasili kwenye maskani yake katika kambi ya wakimbizi wa ndani kwa ndani pale Soweto. Pale, aliteleza na kuanguka kwenye mtaro ya maji taka. “Auuuwi!.... Auuuwi! Mama Wanjiru bwana yako ameingia kwenye mtaro. Njoo tumsaidie” mama mmoja msamaria mwema alipaza sauti na kuvutia umati.
SHUKRAN!!!!
Wakati haya yakijiri, ndoto ya matukio yaliyotendeka kabla ya masaibu haya kumpata Matendechere yalivamia mawazo yake. Akilini, alijaribu kukusanya picha hizo bila ya kitendawili cha asili ya maumivu yake kuteguka.
Midundo mizito ya rumba ilizidi kufagilia katika mkahawa maarufu wa ‘tamasha’ katika barabara ya tugawe umaskini. Kama kuchokoza wenye kuneng’ua viuno kwenye sakafu, Deejay Manyoya aliwachilia kibao maarufu ‘I,m not sober’ cha bendi maarufu ya Jamnazi Afrika. Kauli hii ilisindikizwa na vifijo na nderemo. ungedhani ni karamu ya kukaribisha kurudi kwa Yesu. Haya yakijiri, baadhi ya wenyeji walizidi kumimina chupa za mvinyo macho wakibandika kwenye runinga.
Wakati huu wote, Mzee Matendechere alikuwa amechokorwa kichwa na mizimwi ya mvinyo kiasi ya kwamba aliridhia kutafuta starehe kwenye kochi kando ya ‘counter’.
Ukitizama kushoto, ungeona kundi la makahaba ambao walikuwa wamejikwatua kwatu kwatu wakianika mitego yao tayari kunasa wateja. Mwingine alivalia ‘tumbo cut’ ya kubana kifua yenye maandishi “usiseme maziwa, sema ngombe”. Isitoshe, alivalia sketi fupi iliyofichua mapaja yake yenye madoadoa utadhani ni wa jamii ya chui au fisi.
Wakati viumbe hawa wakisasambua mapaja yao kwa wapita njia, Mzee Matendechere alibakia kuvuta mabaki ya sigara yaliyoangushwa na wateja sakafuni. Baba mtu alizubaishwa na vimulimuli vya taa ya ‘disco light’ akakaribisha moshi ndani ya mapafu kabla ya kuwachilia wingu kubwa hewani.
“Mzee! Inuka uende nyumbani. Tuko karibu kufunga na hatutaki ukamatwe na polisi” wahudumu pale kwenye mkahawa walimrai. “Kwani huyo Mututho anadhani ni nani atupimie starehe na pesa tunakunywa ni zetu? Leta kingfisher mbili hapo.” alisikika Matendechere akizusha kwa ujeuri huku akilaani mbunge aliyebuni sheria inayopima masaa ya kunywa pombe.
Wakati Matendechere akizizana na wale wahudumu , ghafla fikra zake zilivutiwa na maandishi FulanI ukutani. “Customers have a right to stay and to pay”. “Haya ndiyo madhara ya kususia masomo mapema. Can you please read the bold writings on the wall?” Mzee Matendechere aliwakabili huku akionekana kuzidiwa na kichefuchefu.
Kwa dakika zile chache, baba mtu alijiona jogoo wa kukomaa. kuwika kwake kuliwatisha wahudumu. Kwenye lango kuu la mkahawa, tayari wateja wengine wangeonekana wakiondoka wameshikana taratibu kumaanisha walikuwa wameona dalili ya . Kadri masaa yalivyoyoma ndivyo shughuli zilipungua pale hata mziki ikazimwa na stima kuzimwa.
“Ala! Mzee, hii ni siku ya pili tunakutoa hapa kwa nguvu. Kwani huna familia? Enda nyumbani tunafunga.” Askari aliyeshika doria langoni alimzomea Matendechere.
Baadaye, baba mtu aliona amezidiwa maarifa hata akajikusanya na kutembea taratibu akieleka nyumbani. Barabarani, hungempita bila ya kumtambua kutokana na kuimba kwake. “I,m not sober Odiero, I,m not sober……..i,m not sober because I,ve taken guiness.”hivyo ndivyo hali ilikuwa.
Ilibakia kona moja tuu kabla ya kuwasili kwenye maskani yake katika kambi ya wakimbizi wa ndani kwa ndani pale Soweto. Pale, aliteleza na kuanguka kwenye mtaro ya maji taka. “Auuuwi!.... Auuuwi! Mama Wanjiru bwana yako ameingia kwenye mtaro. Njoo tumsaidie” mama mmoja msamaria mwema alipaza sauti na kuvutia umati.
SHUKRAN!!!!
Comments