Skip to main content

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU “SEASON TWO”


“Darling funga macho nikuambie kitu” Bahati alinishurutisha kwa sauti ya upole. Bila kusita, nilifikicha macho yangu kwa viganja vya mkono nikiwa na hamu ya kujua kilichokuwa chaningoja.

Bahati alikuwa na uzoefu wa kunifanyia utani wa aina hii haswa wakati penzi lilkuwa limemchachawiza. Mara ya mwisho alitumia mbinu hii, ni wakati aliponiletea pete ya dhahabu afisini.

Wakati nilipokuwa nimeziba macho, mawazo mengi yaligongana akilini. “labda ana siri Fulani anataka kunieleza ama ni zawadi anataka kunipa? aaah! Potelea mbali, liwe liwalo!” nilijisemeza moyoni.

Ghafla, Mlipuko mkubwa ulisikika hatua chache. sekunde kadhaa baadaye, nilijipata nimelala kifudifudi ardhini huku shati yangu ikitoja damu. “Mungu wangu! Mungu wangu! ” nilibaki kupiga kite huku nikichirizikwa ovyo na damu utosini.

Nilikazana kulinda nguvu kiasi niliyokuwa nimebaki nayo, macho yangu yalipepesa na kuranda randa ovyo nikitafuta alipokuwa Bahati wangu. Mita chache, niliona mawimbi ya bahari yenye hasira yakifagia ufuo na kubingirisha mwili wa mpenzi wangu kuelekea maji makuu.

Nilijaribu kupiga kamsa angalau kuita usaidizi lakini, maghala ya nguvu mwilini yalikuwa tupu. Nilibaki tuu kutizama bahari ikininyanganya kipenzi changu. Ghafla giza nene ilinijia hata nikapoteza fahamu nisipate kujijua.

********************

“Rashidy……………Mzalendo” sauti dhabiti ilinizindua kutoka ule usingizi mzito. “Naam! Ni mimi!” niliitika kwa utiifu, ungedhani nimeitiwa zawadi.

Mawazo yangu yalikuwa yangali yana randa randa. Kufumba na kufumbua nilijipata katika wodi ya wagonjwa mahututi. Kichwa kilikuwa kizito ungedhani limefungiwa gunia ya chumvi.

Pembezoni mwa kitanda, niliona kibuyu fulani kama kibofu ambayo ilikuwa imeshiba damu hata nikadhani naota. “What am I doing in this hospital?” kimombo kilifufuka kinywani.

“Ukweli ni kwamba, umekuwa katika wodi hii kwa miezi miwili sasa. Hii baada ya kujeruhiwa vibaya katika shambulizi la kigaidi lililotekelezwa katika hoteli fulani jijini humu. Habari njema ni kwamba angalu umepata fahamu” jamaa mrefu mwenye surupwenye nyeupe pepepe aliniarifu kwa sauti nyenyekevu.

“Where is my Bahati?” zimwi la kimombo lilivamia usemi wangu tena.
Hata kabla ya kupewa jibu kwa swali hilo, tayari picha za kumbukumbu za Bahati wangu zilikuwa zinapishana akilini. Nilijaribu kuzikusanya picha hizo kujua alivyovalia mara ya mwisho tulipokutana lakini singekumbuka.

“We are very sorry to inform you that your lovely Bahati is no more” maneno yale yalipenyeza akilini kama upanga mkali. Tumboni, ningesikia ngurumo fulani kama radi ambayo iliharibia hata minyoo starehe.

Baadaye, nilishindwa kuhimili uzito wa ujumbe ule hata hewa ikanikatikia. “Haraka! Mlete mtambo ya oxigeni tutampoteza jamaa huyu, hurry up! You bustards” daktari alisikika akiwafokea wauguzi.

ENDELEA KUFUATA HADITHI HII YA KUSISIMUA!!!!!!!!!!

Comments

Anonymous said…
hope you dont wake up soon coz i cant wait for season three
kaka! shukran tena kwa kuendela kujipatia uhondo katika ukurasa huu.
my say my take said…
EBU TOA SEASON THREE MBIO ITS NYC
season three itakujia hivi punde endelea kudurusu ukurasa huu ujue ni kwa nini kiswahili chafaa kupewa heshima kuu!

Popular posts from this blog

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta. Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho. Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni . Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo. “Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa...

SIRI ZA “JAM” JIJINI NAIROBI; TOLEO LA PILI

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Jinsi basi lilivyozidi kufukuzia kuelekea mzunguko wa Nyayo stadium, ndivyo ilizidi kuwachilia moshi ya mpingo iliyosokota angani kabla ya kutawanyika. Pale pia, tulimpata polisi wa trafiki mwanamke aliyefungia mshipi wa longi yake kwenye kifua. Amini usiamini, kwa ishara ya mkono alielekeza mkondo wa gari kama jinsi upepo huele ... keza bendera. Pale tulis...imama kwa dakika chache kabla ya msongamano kufunguliwa. Cha kuvutia tamaa ya macho yangu ilikuwa ‘tuk tuk’ fulani ambayo ilipenya penya kati kati ya magari huku ikipiga kelele kama mashine ya kusaga mahindi. Wenzangu wanaiita kule bara POSHOMILL. “We! Boss, ondoa hiyo kabati kwenye barabara” alisikika akishambuliwa na mmoja wa madereva wa matatu. Wanasema muungwana hununa moyoni na wala siyo mashavuni na kwa hivyo Yule dereva wa ‘tuk tuk’ akaridhia kumjibu kwa kimya. Kando na tukio hili, kuna jambo lililotendeka ambalo liliwacha mbavu za kila mtu zikiuma. Niseme nisiseme! Aaaah! ...