Skip to main content

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU “SEASON TWO”


“Darling funga macho nikuambie kitu” Bahati alinishurutisha kwa sauti ya upole. Bila kusita, nilifikicha macho yangu kwa viganja vya mkono nikiwa na hamu ya kujua kilichokuwa chaningoja.

Bahati alikuwa na uzoefu wa kunifanyia utani wa aina hii haswa wakati penzi lilkuwa limemchachawiza. Mara ya mwisho alitumia mbinu hii, ni wakati aliponiletea pete ya dhahabu afisini.

Wakati nilipokuwa nimeziba macho, mawazo mengi yaligongana akilini. “labda ana siri Fulani anataka kunieleza ama ni zawadi anataka kunipa? aaah! Potelea mbali, liwe liwalo!” nilijisemeza moyoni.

Ghafla, Mlipuko mkubwa ulisikika hatua chache. sekunde kadhaa baadaye, nilijipata nimelala kifudifudi ardhini huku shati yangu ikitoja damu. “Mungu wangu! Mungu wangu! ” nilibaki kupiga kite huku nikichirizikwa ovyo na damu utosini.

Nilikazana kulinda nguvu kiasi niliyokuwa nimebaki nayo, macho yangu yalipepesa na kuranda randa ovyo nikitafuta alipokuwa Bahati wangu. Mita chache, niliona mawimbi ya bahari yenye hasira yakifagia ufuo na kubingirisha mwili wa mpenzi wangu kuelekea maji makuu.

Nilijaribu kupiga kamsa angalau kuita usaidizi lakini, maghala ya nguvu mwilini yalikuwa tupu. Nilibaki tuu kutizama bahari ikininyanganya kipenzi changu. Ghafla giza nene ilinijia hata nikapoteza fahamu nisipate kujijua.

********************

“Rashidy……………Mzalendo” sauti dhabiti ilinizindua kutoka ule usingizi mzito. “Naam! Ni mimi!” niliitika kwa utiifu, ungedhani nimeitiwa zawadi.

Mawazo yangu yalikuwa yangali yana randa randa. Kufumba na kufumbua nilijipata katika wodi ya wagonjwa mahututi. Kichwa kilikuwa kizito ungedhani limefungiwa gunia ya chumvi.

Pembezoni mwa kitanda, niliona kibuyu fulani kama kibofu ambayo ilikuwa imeshiba damu hata nikadhani naota. “What am I doing in this hospital?” kimombo kilifufuka kinywani.

“Ukweli ni kwamba, umekuwa katika wodi hii kwa miezi miwili sasa. Hii baada ya kujeruhiwa vibaya katika shambulizi la kigaidi lililotekelezwa katika hoteli fulani jijini humu. Habari njema ni kwamba angalu umepata fahamu” jamaa mrefu mwenye surupwenye nyeupe pepepe aliniarifu kwa sauti nyenyekevu.

“Where is my Bahati?” zimwi la kimombo lilivamia usemi wangu tena.
Hata kabla ya kupewa jibu kwa swali hilo, tayari picha za kumbukumbu za Bahati wangu zilikuwa zinapishana akilini. Nilijaribu kuzikusanya picha hizo kujua alivyovalia mara ya mwisho tulipokutana lakini singekumbuka.

“We are very sorry to inform you that your lovely Bahati is no more” maneno yale yalipenyeza akilini kama upanga mkali. Tumboni, ningesikia ngurumo fulani kama radi ambayo iliharibia hata minyoo starehe.

Baadaye, nilishindwa kuhimili uzito wa ujumbe ule hata hewa ikanikatikia. “Haraka! Mlete mtambo ya oxigeni tutampoteza jamaa huyu, hurry up! You bustards” daktari alisikika akiwafokea wauguzi.

ENDELEA KUFUATA HADITHI HII YA KUSISIMUA!!!!!!!!!!

Comments

Anonymous said…
hope you dont wake up soon coz i cant wait for season three
kaka! shukran tena kwa kuendela kujipatia uhondo katika ukurasa huu.
my say my take said…
EBU TOA SEASON THREE MBIO ITS NYC
season three itakujia hivi punde endelea kudurusu ukurasa huu ujue ni kwa nini kiswahili chafaa kupewa heshima kuu!

Popular posts from this blog

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

OPERATION TUTETEE WANAUME!!!

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL SEHEMU YA KWANZA: Mzee Matendechere alionekana kuokotwa na usingizi mwepesi wakati akiuguza majeraha ya panga hospitalini. Kisa na maana, adabu ilimhama mkewe hata akaamua kuchukua sheria mkononi na kumpa mumewe kichapo cha mbwa kabla ya kutorokea kusichojulikana. Kichwa chake kilibanwa kwa kilemba cheupe chenye matone ya dam u. Isitoshe, Kwenye shavu la kushoto, palidhihirika jeraha bichi lenye kushonwa kwa uzi. Cha kusikitisha zaidi, Pembezoni mwa kitanda, wangeonekana wapiga picha kutoka vyumba vya habari waking’ang’ana kuchukua picha za kuvutia watazamaji. picha kwa hisani ya http://medievalminds.com Maskini Matendechere alizidiwa na usingizi hata akabakia kukoroma huku akifungua mdomo mithili ya mamba mwenye njaa. “Wow! This seems to be the best shot, I,m loving this” alisikika akisema mmoja wa wapigaji picha tuliyeshuku ni wa asili ya kimarekani. Kweli, vita vya panzi furaha ya kunguru. Wakati haya yakijiri, ndoto ya m...

KUMBU KUMBU ZA MWANA HAWA

MTUNZI: Odhiambo Danyell Manyunyu mepesi ya mvua yangesikika yakikung’uta mabati na kuibua mdundo flani iliozidisha tamaa yangu ya  kuendelea kupanga mbavu kwenye kitanda. Mara, alisikika jogoo mmoja kijijini akiwika kama kuashiria nuru ilikuwa imekubali zamu yake ya mchana. Nilibaki kugaragara kitandani huku mabishano makali yakiendelea akilini kati ya mwili dhaifu na nafsi yangu. Mwili ilisisitiza niendelee kulala huku nafsi ikinisihi niamke. Baada ya kutafakari kuhusu hasara za usingizi niliridhia kuamka. Ghafla, fikra zangu zilielekezwa katika saa kubwa iliyoning'inia ukutani ambayo ilikatiza hali ya unyamafu uliokuwa umetawala chumbani. kuzidisha, chenene fulani aliyekuwa kajificha mvunguni alianza kutoa sauti ya kuudhi. “Aah! Heri tuu niamke” nilijisemeza huku nikijikokota kuelekea kwenye dirisha. Nikichungulia nje, ningeona kunguru wakipigania makombo ya chakula kwenye pipa iliyosimama mkabala na chumba changu. Isitoshe, rukwama kukuu za wazegaz...