Skip to main content

FEDHEHA ZA SWALEH

MTUNZI: MARIA REHEMA

Swaleh kijana wa miaka ishirini na tisa alienda usingizini, akiwaza na kuwazua jinsi atakavyo jishindia jiko. Alihesabu miaka yake na kustaajabu kuwa miaka hiyo yote, alikuwa anavunda upweke. Kisa na maana hakuwa na bila barafu wa roho.

Liwike lisiwike kutakucha. Swaleh aliamka na kabla ya kupata staftahi, alianza siku kwa kujipodoa. Liche ya uzito wake na kipipa cha tumbo, aliamua kuvaa shati na suruale iliyombana kupindukia. “ Ndo mavazi ya kisasa haya, nitaweza kuwapata warembo kadhaa,” alijiambia Swaleh.

Baada ya staftahi, Swaleh huyo kiguu na njia jijini kutafuta kipenzi cha roho. Bak bandika bak bandua mpaka kwenye kituo cha basi. Alipoingia kwenye ‘matatu’ moja akakutana na kidosho aliyerembeka mno.

Hakupoteza wakati alikimbia na kuketi karibu na mrembo huyo. Alivutiwa na macho yake makubwa yaliyong’aa na ngozi yake nyororo. Mwili wake je? Nikisema zaidi utamwonea wivu. Maumbile haya yalimtia Swaleh wazimu.

Bila shaka Swaleh alibaki mdomo wazi maneno yakimganda kinywani. Dakika kumi zilipita kama bado wawili hao hawajaongea. Swaleh alikuwa akimeza mate tu huku akimrushia kijicho cha tamaa. Matatu lilipofika jijini wawili hawa walishuka.

Msichana huyo aliposhuka aliangusha mkoba wake. Swaleh huyooo! Alitaka kuonyesha hisani na kwa hivyo hakusita kutoa msaad.

Alipoinama kuuchukua mfuko huo, ghafla! suruali yake iliraruka huko nyuma asijue la kufanya. ikiwa ulisoma jiografia utakumbuka chimbuko la bonde la ufa.  Hayo kando, mara Swaleh aliamka mbio kujiangalia huku haya ikimvaa usoni. Watu walioshuhudia tukio hilo hawangejizuia kicheko.


Kama kusugua chumvi kwenye kidonda, mara  kifungo cha suruali ya Swaleh iling’oka na kuruka kumwahi mwanamke mkongwe aliyekuwa katika umati uliomzingira. Swaleh aliinama ili kuzuia suruali yake kumvuka. Lakini aibu haijui be wala te, suruali iliraruka zaidi. 

Alichana mbuga na kuiingia na kuingia katika “ Public toilet”. Baada ya aibu hiyo, alijihisi kuenda msalani. Majasho yalikuwa yamemtoka midhili ya maji mferejini. Alipomaliza kujisaidia alienda kunawa mikono. Punde tu, alipofunguwa mfereji, maji yakatoka na fujo kumtoteshea upande wote wa mbele ya suruale yake.
 “Salala! Aibu gani hii, si nguo zangu kuraruka, sasa nimetota.” Swaleh alilia.

Alipokuwa njiani kwenda kwake, kila aliyempita Swaleh angedhania amejikojolea. Alipofika nyumbani kwake, aliufunga mlango wake na kufuli na kuketi chini. Alitafakari jinsi tamaa yake ya kupata mke ilivyomletea aibu mno. 

Usiku ulipofika, alijisongea sima na kukaanga mboga na akala. Alipokula, aliingia chumbani na kupanda kitandani akingoja usingizi umchukue. 
… katika kipindi kijayo cha Fedheha za Swaleh. 
“ Mwanangu huji kumtembelea mamako siku hizi?” Swabaha alilia.

Comments

Popular posts from this blog

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

OPERATION TUTETEE WANAUME!!!

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL SEHEMU YA KWANZA: Mzee Matendechere alionekana kuokotwa na usingizi mwepesi wakati akiuguza majeraha ya panga hospitalini. Kisa na maana, adabu ilimhama mkewe hata akaamua kuchukua sheria mkononi na kumpa mumewe kichapo cha mbwa kabla ya kutorokea kusichojulikana. Kichwa chake kilibanwa kwa kilemba cheupe chenye matone ya dam u. Isitoshe, Kwenye shavu la kushoto, palidhihirika jeraha bichi lenye kushonwa kwa uzi. Cha kusikitisha zaidi, Pembezoni mwa kitanda, wangeonekana wapiga picha kutoka vyumba vya habari waking’ang’ana kuchukua picha za kuvutia watazamaji. picha kwa hisani ya http://medievalminds.com Maskini Matendechere alizidiwa na usingizi hata akabakia kukoroma huku akifungua mdomo mithili ya mamba mwenye njaa. “Wow! This seems to be the best shot, I,m loving this” alisikika akisema mmoja wa wapigaji picha tuliyeshuku ni wa asili ya kimarekani. Kweli, vita vya panzi furaha ya kunguru. Wakati haya yakijiri, ndoto ya m...

KUMBU KUMBU ZA MWANA HAWA

MTUNZI: Odhiambo Danyell Manyunyu mepesi ya mvua yangesikika yakikung’uta mabati na kuibua mdundo flani iliozidisha tamaa yangu ya  kuendelea kupanga mbavu kwenye kitanda. Mara, alisikika jogoo mmoja kijijini akiwika kama kuashiria nuru ilikuwa imekubali zamu yake ya mchana. Nilibaki kugaragara kitandani huku mabishano makali yakiendelea akilini kati ya mwili dhaifu na nafsi yangu. Mwili ilisisitiza niendelee kulala huku nafsi ikinisihi niamke. Baada ya kutafakari kuhusu hasara za usingizi niliridhia kuamka. Ghafla, fikra zangu zilielekezwa katika saa kubwa iliyoning'inia ukutani ambayo ilikatiza hali ya unyamafu uliokuwa umetawala chumbani. kuzidisha, chenene fulani aliyekuwa kajificha mvunguni alianza kutoa sauti ya kuudhi. “Aah! Heri tuu niamke” nilijisemeza huku nikijikokota kuelekea kwenye dirisha. Nikichungulia nje, ningeona kunguru wakipigania makombo ya chakula kwenye pipa iliyosimama mkabala na chumba changu. Isitoshe, rukwama kukuu za wazegaz...