MTUNZI: MARIA REHEMA
Swaleh kijana wa miaka ishirini na tisa alienda usingizini, akiwaza na kuwazua jinsi atakavyo jishindia jiko. Alihesabu miaka yake na kustaajabu kuwa miaka hiyo yote, alikuwa anavunda upweke. Kisa na maana hakuwa na bila barafu wa roho.
Liwike lisiwike kutakucha. Swaleh aliamka na kabla ya kupata staftahi, alianza siku kwa kujipodoa. Liche ya uzito wake na kipipa cha tumbo, aliamua kuvaa shati na suruale iliyombana kupindukia. “ Ndo mavazi ya kisasa haya, nitaweza kuwapata warembo kadhaa,” alijiambia Swaleh.
Baada ya staftahi, Swaleh huyo kiguu na njia jijini kutafuta kipenzi cha roho. Bak bandika bak bandua mpaka kwenye kituo cha basi. Alipoingia kwenye ‘matatu’ moja akakutana na kidosho aliyerembeka mno.
Hakupoteza wakati alikimbia na kuketi karibu na mrembo huyo. Alivutiwa na macho yake makubwa yaliyong’aa na ngozi yake nyororo. Mwili wake je? Nikisema zaidi utamwonea wivu. Maumbile haya yalimtia Swaleh wazimu.
Bila shaka Swaleh alibaki mdomo wazi maneno yakimganda kinywani. Dakika kumi zilipita kama bado wawili hao hawajaongea. Swaleh alikuwa akimeza mate tu huku akimrushia kijicho cha tamaa. Matatu lilipofika jijini wawili hawa walishuka.
Msichana huyo aliposhuka aliangusha mkoba wake. Swaleh huyooo! Alitaka kuonyesha hisani na kwa hivyo hakusita kutoa msaad.
Alipoinama kuuchukua mfuko huo, ghafla! suruali yake iliraruka huko nyuma asijue la kufanya. ikiwa ulisoma jiografia utakumbuka chimbuko la bonde la ufa. Hayo kando, mara Swaleh aliamka mbio kujiangalia huku haya ikimvaa usoni. Watu walioshuhudia tukio hilo hawangejizuia kicheko.
Swaleh kijana wa miaka ishirini na tisa alienda usingizini, akiwaza na kuwazua jinsi atakavyo jishindia jiko. Alihesabu miaka yake na kustaajabu kuwa miaka hiyo yote, alikuwa anavunda upweke. Kisa na maana hakuwa na bila barafu wa roho.
Liwike lisiwike kutakucha. Swaleh aliamka na kabla ya kupata staftahi, alianza siku kwa kujipodoa. Liche ya uzito wake na kipipa cha tumbo, aliamua kuvaa shati na suruale iliyombana kupindukia. “ Ndo mavazi ya kisasa haya, nitaweza kuwapata warembo kadhaa,” alijiambia Swaleh.
Baada ya staftahi, Swaleh huyo kiguu na njia jijini kutafuta kipenzi cha roho. Bak bandika bak bandua mpaka kwenye kituo cha basi. Alipoingia kwenye ‘matatu’ moja akakutana na kidosho aliyerembeka mno.
Hakupoteza wakati alikimbia na kuketi karibu na mrembo huyo. Alivutiwa na macho yake makubwa yaliyong’aa na ngozi yake nyororo. Mwili wake je? Nikisema zaidi utamwonea wivu. Maumbile haya yalimtia Swaleh wazimu.
Bila shaka Swaleh alibaki mdomo wazi maneno yakimganda kinywani. Dakika kumi zilipita kama bado wawili hao hawajaongea. Swaleh alikuwa akimeza mate tu huku akimrushia kijicho cha tamaa. Matatu lilipofika jijini wawili hawa walishuka.
Msichana huyo aliposhuka aliangusha mkoba wake. Swaleh huyooo! Alitaka kuonyesha hisani na kwa hivyo hakusita kutoa msaad.
Alipoinama kuuchukua mfuko huo, ghafla! suruali yake iliraruka huko nyuma asijue la kufanya. ikiwa ulisoma jiografia utakumbuka chimbuko la bonde la ufa. Hayo kando, mara Swaleh aliamka mbio kujiangalia huku haya ikimvaa usoni. Watu walioshuhudia tukio hilo hawangejizuia kicheko.
Kama kusugua chumvi kwenye kidonda, mara kifungo cha suruali ya Swaleh iling’oka na
kuruka kumwahi mwanamke mkongwe aliyekuwa katika umati uliomzingira. Swaleh aliinama
ili kuzuia suruali yake kumvuka. Lakini aibu haijui be wala te, suruali
iliraruka zaidi.
Alichana mbuga na kuiingia na kuingia katika “ Public toilet”. Baada ya aibu hiyo,
alijihisi kuenda msalani. Majasho yalikuwa yamemtoka midhili ya maji mferejini.
Alipomaliza kujisaidia alienda kunawa mikono. Punde tu, alipofunguwa mfereji,
maji yakatoka na fujo kumtoteshea upande wote wa mbele ya suruale yake.
“Salala! Aibu gani hii, si nguo zangu
kuraruka, sasa nimetota.” Swaleh alilia.
Alipokuwa njiani kwenda kwake, kila aliyempita
Swaleh angedhania amejikojolea. Alipofika nyumbani kwake, aliufunga mlango wake
na kufuli na kuketi chini. Alitafakari jinsi tamaa yake ya kupata mke
ilivyomletea aibu mno.
Usiku ulipofika, alijisongea sima na kukaanga mboga
na akala. Alipokula, aliingia chumbani na kupanda kitandani akingoja usingizi
umchukue.
… katika kipindi kijayo cha Fedheha za
Swaleh.
“ Mwanangu huji kumtembelea mamako siku hizi?”
Swabaha alilia.
Comments