MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL
Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta.
Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho.
Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni.
Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo.
“Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa mbali, nilimsikia Bahati wangu akiita. Nilipogeuka nilimwona akiruka huku akirusha mkono kama kunisihi niende alipokuwa.
Nikivalia makubadhi ,suruali fupi ya samawati na shati yenye michoro ya vibonzo na taratibu nikateremka kwenye ngazi ya mbao. badaye nilifuata njia ya nyasi iliyochongwa kando kando kuelekea alipokuwa mpenzi wangu.
Bila kusita alikimbia na kunirukia kwenye mabega huku akizamisha busu moto kwenye shavu langu. Hisiya kweli hazifungiwi mlango………………………endelea kutembelea ukurasa huu ujue yapi yatatokea katika hadithi hii
Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta.
Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho.
Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni.
Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo.
“Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa mbali, nilimsikia Bahati wangu akiita. Nilipogeuka nilimwona akiruka huku akirusha mkono kama kunisihi niende alipokuwa.
Nikivalia makubadhi ,suruali fupi ya samawati na shati yenye michoro ya vibonzo na taratibu nikateremka kwenye ngazi ya mbao. badaye nilifuata njia ya nyasi iliyochongwa kando kando kuelekea alipokuwa mpenzi wangu.
Bila kusita alikimbia na kunirukia kwenye mabega huku akizamisha busu moto kwenye shavu langu. Hisiya kweli hazifungiwi mlango………………………endelea kutembelea ukurasa huu ujue yapi yatatokea katika hadithi hii
Comments