MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Wa kwanza alikuwa Rehema, njia zetu zilikutana kwenye ufuo wa bahari hindi msimu wa upanzi wa mwaka 1999. Kidonda hicho kingali kibichi. Japo nilibaki na kovu, nahisi ni kama nazungumzia ya jana. Kwa ufupi, yake na yangu yalikuwa mafupi hata ingawa vioja vilikuwa teletele. Uhusiano wa kunoga tulilinda kwa takriban miezi miwili. Siku moja, aliamka na kuniambia yu mja mzito. Nilimshauri akakiangamize kijusi hicho. Hii ilitokana na wingi wa uoga kuhusu majukumu ambayo yangendamana na hali hiyo. Alikubali wito japo shingo upande. Baadaye, niliarifiwa yuko hali mahututi katika katika zahanati ya Dr. Tiba wa Maradhi. Kesho yake Jioni , nilipata simu ya dharura. “harakisha mpenzio amevuja damu nyingi sana akijaribu kuavya mimba changa. Nasikitika kusema, si wa dunia hii tena.” hitimisho likawa ni maombolezi na baadaye mazishi huku vidole zote nikielekezewa. Vivyo hivyo, aliyefuatilia mkondo huu alikuwa kipusa kwa jina Amina. Mtoto yatima ambaye nilipata kum...
MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL CHUO KIKUU CHA DAYSTAR NAIROBI Magurudumu ya matatu yalikimbizana kuelekea kwenye lango kuu la ziwa Baringo. Nyuma yetu barabara ilikuwa safi japo kwa vumbi nyepesi pamoja na moshi ambayo ilionekana kutuandama kabla ya kusokota angani. Pembeni mwa lango hilo, palisimama wima kibao “Welcome to Lake Baringo” hii ikawa ni ridhisho tosha kwamba makaribisho kabambe yalikuwa yatungoja. Kama ada, tuliegesha gari mbele ya kizuizi cha baraza la jiji. yaliyofuata, yakawa ni kuhesabiwa kisha kulipia kiingilio. “Karibuni na mjienjoy kabisa” askari kwenye lango alitueleza. Baadaye, kizuizi kiliinuliwa kuashiria tulikuwa huru kuvinjari kila kona ya ziwa ambalo nilikuwa nimesikia tuu kupitia uvumi wa marafiki pamoja na maarifa ya vitabu za jiografia. Kuonekana kwa ziwa upeoni kuliwafanya hata waliokuwa wanasinzia kupata sababu ya kuchangamka. “Lake Baringo here we come!” kidosho aliyekuwa kando yangu alisema wakati akingangana kupiga picha kutumia si...