Skip to main content

SIRI ZA 'JAM' JIJINI NAIROBI

MTUNZI:ODHIAMBO DANYELL

Dereva wa basi la kampuni ya RWAKEN alijistiri mbele ya usukani na kupiga gari moto wakati tukiondoka katika kitivo cha chuo kikuu cha Daystar yenye makao katika mzunguko wa barabara ya Valley road, Nairobi.

Ilikuwa dakika chache baada ya saa kumi na nusu jioni. Hii ni kumaanisha, wafanyikazi pamoja na wanafunzi wa mchana chuoni tayari walikuwa katika harakati zakufunganya virago na kurejea makwao baada ya panda shuka za mchana.


Vvrrrrrrrrrrrrrm! vvrrrrrrrm! Dereva alipasha gari moto na taratibu basi likaelekezwa nje ya lango kuu. kabla ya kuingia kwenye barabara kuu ya Valley road.

Auuuuuwi! imagine mbele yetu palisimama gari aina ya Range Rover Vogue iliyowachilia moshi nyeupe iliyosokota na kupata hifadhi katika mapua ya basi la RWAKEN. Katika mbuga la wanyama, gari hili linalinganishwa na mfalme Simba kutokana na udhabiti wake. Mashini hii yasifika kwa ulafi wa petroli pamoja na muundo wake wa kutamanisha. Aha! Sasa nimejua kwanini basi ilikuwa inanguruma kama yenye mafua....

Kando na hayo, sisemi nilivutiwa zaidi na rangi yake nyekundu ya kukoza pamoja na ‘rims’ za shaba ukipenda silver na isitoshe magurudumu inchi sita. Kutamanisha zaidi, ilikuwa nambari yake ya usajili KBR 001Z. “Bonge la wallpaper” alisikika mmoja akishangaa ndani ya basi.

Kushoto, palinguruma gari nyingine aina ya Hummer, almaarufu ‘nyundo’. huyu pia ni Ibilisi mwingine katika orodha ya maadui wa petroli. Nikimwita kifaru wa jiji hutanipinga. Maumbile yake, pamoja nasifa yake ya  kutembea kifua mbele inalingana na ubingwa wake.

Mbele alirembeshwa kwa vyuma vya kumetameta. Nyuma alikosa nambari ya usajili hata tukashuku bado mgeni nchini. Kitendawili kumhusu ni uhusiano wake kimapenzi na wanasiasa nchini Kenya.ukitaka umaarufu huna budi kumchombeza.

Kwenye msafara, alifanya magari mengine ya kibinafsi kuonekana kama siafu. sitataja kina kaka Vitz, Alex,Runx, March, Probox orodha ni ndefu taja zingine........

Tuwache hayo. kuna huyu dereva wa vitz aliyeonekana kuwa na haraka na hata akapenyeza kijigari lake kwenye njia ya mguu kando kando hata kuwaudhi wapita njia. utanikashifu kwa kuwa mmbea lakini heri nimfichue.

Hayawi hayawi, hatimaye huwa. Polisi wa trafiki mwenye kitumbo cha kiriba alifungulia magari na taratibu msafara wa magari ulisonga kama jinsi mkondo wa mto huteremka mlima. Ghafla, mkondo ulishika kasi na magari yakapepea kwenye barabara kuu ya mbagathi.

Tulipofikia makutano ya barabara ya Langata, tulipata pamefanyika ajali mbaya sana. Kulingana na mashahidi wa karibu, dereva wa gari hilo aina ya Toyota Caldina alisemekana kupoteza mwelekeo kabla ya kurukia gomba la ndizi kando ya barabara. Gari ilijikunja sura ungedhani imepiga busu domo la gari moshi. "Wololo! Maskini!" alishangaa dereva wa basi.


Comments

Popular posts from this blog

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta. Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho. Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni . Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo. “Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa...

SIRI ZA CHUO KIKUU CHA DAYSTAR

Njoo unisome kwa makini S.L.P 927 MACHO PLAZA Kwa wewe unayenisoma, Habari za utokako? Naona unahema kweli ukitaka kujua yaliyojiri hivi leo kwenye barua hii. Hee! By the way, ikiwa wataka tuelewane naomba uwache kuniangalia kwa hizo macho za kushiba chuki na dharau. Kabla nikuendelezee udaku! Tafadhali wacha kuangalia kando kando ukinisoma. Unawafanya wapita njia wanadhani tunawasengenya humu. By the way, usha ambiwa na yeyote hivi leo kwamba watamanisha? Ooooooooooooh! Nisamehe. I mean.... you are fearfully and wonderfully made. Sitaongeza wala sitapunguza. Niwie radhi siwes kutranslate, please! Mwelezee.. aliye kando yako aje akusaidie. Kabla nikupatie udaku, natamani niulize swali moja tuu. Nihakikishie kwamba hutanuna! Naogopa lakini heri niulize tuu atleast tusafiane nia. Hivi mbona una blush sana? Kama nimekubamba si uniambie tuu ama uwaite wanafunzi wenzako waje wasome uhondo. Matawi ya miti naona inapukutika kutokana na upepo mkali unaofagilia kutoka milima ya l...