Skip to main content

USHUHUDA WA MKIMBIZI

Januari tarehe 23, 2012
Saa iliyotulia wima kwenye kuta ya hema ilifichua kwamba ilibakia dakika chache kabla ya saa nane mchana . Akilini halikunijia wazo kwamba jaji wa mahakama ya Hague Bi Ekaterina Trendafilova alikuwa anasubiriwa kutoa uamuzi wa korti dhidi ya washukiwa sita wa vita vya baada ya uchaguzi.

Msimu wa masika tayari ulikuwa umeenda likizo, kiangazi kilikuwa kinatawala na umaarufu wa jua kijijini ungedhihirika kwa jinsi miale yake ilizidi kukausha nchi kavu hata nyufa zikatawala ardhini.
 kambi ya wakimbizi ya faraja

Mara kwa mara, tufani kali za kutoka magharibi zingesikika zikifagilia na kufanya matawi ya miembe kupukutika kabla ya kuchezeshwa angani ovyo ovyo. Nilikuwa nimetulia kwenye mkeka ndani ya hema ndipo nikagutushwa na unyamale uliojiri kwenye kambi ya wakimbizi ya faraja. Mara moja, nikashuku hatari na kuchungulia nje angalau kuhakikisha kila kitu kilikuwa sawa.

Nikisimama kwenye mlango ya hema, ningehisi hali isiyo ya kawaida. Upweke ulitawala kote japo kwa ndege ambao walikuwa katika shughuli ya kujenga viota juu ya miembe. Hii ilikuwa tofauti na hali ya kawaida ambapo kelele za majirani zingevunja tamaa ya mtu kutaka kuonja usingizi wakati wa mchana.

Hata kabla ya mate kunikauka mdomoni, upepo mkali ulifagilia na kupepeta kila kitu ndani ya hema hata nikahofia ingeng’oa hema. “shetani ashindwe!” nilitamka maneno hayo kumkemea ibilisi ambaye tuliambiwa huandamana na upepo ya aina hii na kuletea wanadamu nuksi.

Kabla ya fikra zile kunikauka akilini, nilinyongwa na mate nikikadiria madhara ya upepo ule. Picha za familia yangu nilizozistiri kwenye kioo ziliangushwa na vipande vya kioo vikabaki kutapakaa sakafuni.
Picha hizo zilibeba kumbukumbu ya wazazi wangu pamoja na mandugu zangu mapacha ambao waliuliwa kinyama wakati wa machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 nchini Kenya.

Shetani ashindwe!
Ghafla, milango ya machozi ilijiwachilia huru na nikadondokwa na machozi kama kitoto nisijue la kufanya. Nilijihisi ni kama nimedungwa msumari moto kwenye kidonda mbichi. Maumivu yalinizidi hata wazo likanijia la kujitoa uhai kwani uzito huu ulikuwa umelemea mabega yangu.

Nilijiliwaza nikisemeza moyoni. “heri mimi nimebaki na picha, laa sivyo nisingepata fursa kuona sura zao tena baada ya mkasa ule wa moto.” Kila mara nikisema hivi nilihisi nimefarijika kwani mara ya mwisho kuwaona familia yangu ilikuwa mkesha wa siku ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu. Singedhani kwamba katili fulani angefikia kauli ya moto nyumba yetu na kuwabadilisha wote kuwa jivu.


Aha! Kilio cha dakika chache kilisaidia kufungua macho ya ubongo wangu ambayo ilikuwa imeziba. Nilishangaa kamasi nyepesi ikinitoka puani hata nikahitimu kuwa zuzu.

“ Ala! Kumbe leo ni siku ya kutolewa kwa uamuzi wa korti ya kimataifa ya Hague kuhusiana na wale wasita wanaoshukiwa kuchochea vita vya baada ya uchaguzi? No wonder! ” nilijisemeza huku nikingata ulimi.

Kama mwenye kupandwa na kichaa nilijizoa kutoa sakafuni na kupanguza machozi kabla ya kufululiza hadi kwenye ukumbi wa burudani wa pataneni pale kijijini. Nilijua ni hapo pekee ndipo nilikuwa na hakikisho la kupata kutizama televisheni. Pale palifurika furi furi hata nzi hangepata mahala pa kutua salama. Nilijaribu kepenya katikati ya umati lakini lo! Ilishindikana.

Bi Ekaterina Trendafilova asoma uamuzi wa korti!!

“Daima dua la kuku halimpati mwewe” nilisema kimoyomoyo. Hayo ndiyo mawazo yaliyorandaranda akilini wakati Bi Ekaterina Trendafilova aliposoma uamuzi wa koti. Nilijua daima mnyonge hana haki na kwa hivyo nilijitayarisha vilivyo kupokea uamuzi nikijua washukiwa hao wangeondolewa mashtaka.


Ghafla, nilikunakuna sikio alipofikia kilele cha uamuzi kuhakikisha nta haingenizuia kupokea ujumbe ule moja kwa moja. Singeruhusu masikio kuokota uvumi wakati kama huo kwani uamuzi huu ungepelekea kudumisha haki kwa wahasiriwa wa vita hivyo almaarufu Post Election Violence. Angalau usiseme sijui kimombo.

Lililofuata ni ujumbe ambao ulifanya magoti yangu kuingia unyonge kwani wawili kati ya washukiwa wasita walitolewa mashtaka na nikabaki kujua wanne waliobaki pia wangeepuka hivyo tuu!
Katika ukumbi huo singejizuia kuona nyuso za wakimbizi wenzangu ambazo zilitawaliwa na mchanganyiko wa hisiya za ghadhabu pamoja na huzuni huku kope za wengine zikionekana kuloa machozi.

Baadaye ilitangazwa kwamba Hussein Ali pamoja na Henry kosgey walikuwa wameondolewa mashtaka kutokana na uchache wa ushahidi. Kwa upande mwingine, Uhuru Kenyatta, William Ruto, Francis Muthuara na Joshua Arap Sang walijipata matatani  wakielekezwa katika mkondo wa pili wa kudhibitisha kesi dhidi yao.

Ajabu, Minongono ilisikika kichinichini na baadaye kutawala wakati wengi wakionesha kutoridhishwa na uamuzi ule. Sekunde chache baadaye, umati ulifumukana na kila mmoja akaelekea kwake. Kila mmoja alivalia sura ya mazishi.

Adhabu ya mlevi
Kwa umbali, mlevi mmoja alisikika akishangilia uamuzi huo akisema wote hawana hatia ni kusingiziwa tuu. “aaaaaaaaa! Porojo tupu. Hata hao wengine watatolewa tuu mashtaka” alisikika akisema.

“Uuuuuuwi! Uuuuuuwi! Nisaidieni! Nisaidieni!” hiyo ndiyo sauti iliyosikika baadaye. Tulipoharakisha kuelekea palipokuwa na kelele hiyo, tulimpata mlevi huyo amepewa kichapo cha mbwa huku damu ikimtiririka ovyo ovyo.
“Ni nini ya maana kabila zetu ama kudumisha umoja baina ya kabila zetu” aliuliza chifu huku umati ukimjibu kwa sura za mashangao!

Comments

Popular posts from this blog

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

MAPENZI KIZUNGU ZUNGU

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Mawimbi makali baharini yalikimbizana na hatimaye kusukuma maji hadi ufukweni. Pembeni, Bahati alionekana ameshika kijiti kirefu mkononi akijaribu kuchora umbo la moyo wa mapenzi kwenye changarawe mbichi huku maji ya bahari yakifuta. Angani, ndege aina ya korongo na mbayu wayu wangeonekana wakicheza cheza huku tufani kali zikifanya matawi ya minazi ufuoni kupukutika. Nikijistiri juu ya roshani(balcony) katika hoteli ambayo tulikuwa tumekodisha nilisalia kula kwa macho. Nilibakia kinywa wazi kuona madhari ya kutamanisha jinsi jua ilizama upeoni na kufanya maji ya bahari kupiga rangi ya manjano. mawazoni, nilitawaliwa na picha za harusi yetu jana yake katika ukumbi wa pataneni . Hatua chache niliona suti yangu ambayo ilikuwa ingali sakafuni baada ya usiku yenye sarakasi si kidogo. Ajabu, marashi yenye uhai aliyopiga Bahati ilikuwa bado imesakama pua yangu.Waliosema harusi ni kilele cha mapenzi hawakukosea hata kidogo. “Honey…………Rashidy! Rashidy!” Kwa...

SIRI ZA “JAM” JIJINI NAIROBI; TOLEO LA PILI

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Jinsi basi lilivyozidi kufukuzia kuelekea mzunguko wa Nyayo stadium, ndivyo ilizidi kuwachilia moshi ya mpingo iliyosokota angani kabla ya kutawanyika. Pale pia, tulimpata polisi wa trafiki mwanamke aliyefungia mshipi wa longi yake kwenye kifua. Amini usiamini, kwa ishara ya mkono alielekeza mkondo wa gari kama jinsi upepo huele ... keza bendera. Pale tulis...imama kwa dakika chache kabla ya msongamano kufunguliwa. Cha kuvutia tamaa ya macho yangu ilikuwa ‘tuk tuk’ fulani ambayo ilipenya penya kati kati ya magari huku ikipiga kelele kama mashine ya kusaga mahindi. Wenzangu wanaiita kule bara POSHOMILL. “We! Boss, ondoa hiyo kabati kwenye barabara” alisikika akishambuliwa na mmoja wa madereva wa matatu. Wanasema muungwana hununa moyoni na wala siyo mashavuni na kwa hivyo Yule dereva wa ‘tuk tuk’ akaridhia kumjibu kwa kimya. Kando na tukio hili, kuna jambo lililotendeka ambalo liliwacha mbavu za kila mtu zikiuma. Niseme nisiseme! Aaaah! ...