Skip to main content

KUFUNGWA KWA SOKO YA BURMA NI FURAHA WAKAAZI WA NAIROBI

Mtunzi: Odhiambo Danyell

Ni bayana kwamba wenyeji wa Nairobi na vitongoji vyake wana kila
sababu ya kutabasamu baada ya tangazo la kufungwa kwa soko maarufu la
nyama kwa jina Burma. Hatua hii imechochewa na  tabia ya  wafanyi
biashara kukaidi kutii sheria za wakaguzi wa afya.

Kabla ya kungamua hatari inayowakodolea macho walamba minofu katika
soko hilo ni heri nikufafanulie taswira halisi angalau ufahamu
chimbuko la  hatua hii. Punde tuu unapofika katika lango kuu la soko
hilo utakaribishwa na harufu mbaya inayoninginia hewani.

Kando na hayo, utashuhudia jaa kubwa la taka la kusheheni pembe za
wanyama, makombo ya minofu pamoja na maji taka iliyozagaa kila sehemu.
Hatimaye, utawaona chokora wakibishana na mbwa ambao hukukwangura jaa
hilo wakitafuta pato lao.

Kuingia ndani, utapishana na wafanyi biashara wa nyama waliovalia
ovaroli chafu za kutona damu wakibeba bidhaa hiyo kiholela huku
wakivuka mitaro iliyosakamwa na maji taka iliyoganda wakati
wakisindikizwa na vikosi vya nzi.

Aidha, kwenye maduka na hoteli , hutakosa kujionea jeshi kubwa  la nzi
ambao  wameteka nyara kila sehemu hata kuwalazimisha wenyeji kurusha
rusha mikono wakati wakiendelea kufurahia mapishi rojorojo ambayo
huandaliwa kwenye hoteli hizo za Burma.

Tushamhoji mgonjwa na sasa hatuna budi kugeukia daktari angaa tupate
tiba kwa hali hii mbaya kwa vile ni wazi, tusipojenga ufa  tutajenga
ukuta. Hivyo, wakati tukiwakemea wafanyibiahsra wa Burma na kukumbatia
hatua ya kufunga soko hilo ni muhimu mikakati kabambe iwekwe ili
kuepusha wenyeji wa soko hilo na mikurupuko ya magonjwa.

Hayo ni tisa, kumi ni kwamba ili kupata suluhisho la kudumu soko hilo
lafaa kubomolewa na hatimaye kujengwa upya huku wakizingatia miundo
msingi za kuimarisha usafi. Aidha, sheria za baraza la jiji pamoja na
zile za wizara husika zinapaswa kukazwa. Mwisho, wenyeji wanapaswa
kufanyiwa hamasisho kuhusu umuhimu wa kudumisha usafi na hatari ya
kuendelea kufanya kazi zao katika mazingira hayo.

Comments

Popular posts from this blog

MAZINGAOMBWE YA SAA

Na Danyell Odhiambo Nimejirusha kwenye kiti kilegevu cha msonobari nikifikiria jinsi hali ya maisha nchini Kenya inavyozidi kupaa kila uchao. Mbele yangu, pametulia redio, kando pamesimama kikombe cha kahawa chungu na juu pananinginia saa ya ukuta. Ghafla, fikra zangu zinatekwa nyara na saa iliyozubaa ukutani. Nikiangazaangaza, naona imetimia usiku mkuu. Hii ni kumaanisha, mishale yote ya saa imekutana kifuani pa namba kumi na mbili. Ukipiga hesabu kwa makini, utakubalina nami kwamba tukio kama hili hujirudia mara mia tatu sitini na tano kila mwaka. Ukumbuke, kisa hiki pia huashiria kuzaliwa kwa siku mpya. Hata ingawa mishale hizi zimedhibitisha ushirikiano ni kiungo muhimu katika katika kikundi, taswira fulani inaibuka nikiangalia mishale hizo. Taswira yenyewe yahusu tabia mbovu ya wabunge kukaidi shinikizo za kuwataka kulipa malimbikizi yao ya kodi. Nikipamabanua kitendawili hiki, itakubali kwamba jamii imejigawanya kupitia mishale hizi tatu za saa. Mahuluku taabu nawafa...

OPERATION TUTETEE WANAUME!!!

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL SEHEMU YA KWANZA: Mzee Matendechere alionekana kuokotwa na usingizi mwepesi wakati akiuguza majeraha ya panga hospitalini. Kisa na maana, adabu ilimhama mkewe hata akaamua kuchukua sheria mkononi na kumpa mumewe kichapo cha mbwa kabla ya kutorokea kusichojulikana. Kichwa chake kilibanwa kwa kilemba cheupe chenye matone ya dam u. Isitoshe, Kwenye shavu la kushoto, palidhihirika jeraha bichi lenye kushonwa kwa uzi. Cha kusikitisha zaidi, Pembezoni mwa kitanda, wangeonekana wapiga picha kutoka vyumba vya habari waking’ang’ana kuchukua picha za kuvutia watazamaji. picha kwa hisani ya http://medievalminds.com Maskini Matendechere alizidiwa na usingizi hata akabakia kukoroma huku akifungua mdomo mithili ya mamba mwenye njaa. “Wow! This seems to be the best shot, I,m loving this” alisikika akisema mmoja wa wapigaji picha tuliyeshuku ni wa asili ya kimarekani. Kweli, vita vya panzi furaha ya kunguru. Wakati haya yakijiri, ndoto ya m...

KUMBU KUMBU ZA MWANA HAWA

MTUNZI: Odhiambo Danyell Manyunyu mepesi ya mvua yangesikika yakikung’uta mabati na kuibua mdundo flani iliozidisha tamaa yangu ya  kuendelea kupanga mbavu kwenye kitanda. Mara, alisikika jogoo mmoja kijijini akiwika kama kuashiria nuru ilikuwa imekubali zamu yake ya mchana. Nilibaki kugaragara kitandani huku mabishano makali yakiendelea akilini kati ya mwili dhaifu na nafsi yangu. Mwili ilisisitiza niendelee kulala huku nafsi ikinisihi niamke. Baada ya kutafakari kuhusu hasara za usingizi niliridhia kuamka. Ghafla, fikra zangu zilielekezwa katika saa kubwa iliyoning'inia ukutani ambayo ilikatiza hali ya unyamafu uliokuwa umetawala chumbani. kuzidisha, chenene fulani aliyekuwa kajificha mvunguni alianza kutoa sauti ya kuudhi. “Aah! Heri tuu niamke” nilijisemeza huku nikijikokota kuelekea kwenye dirisha. Nikichungulia nje, ningeona kunguru wakipigania makombo ya chakula kwenye pipa iliyosimama mkabala na chumba changu. Isitoshe, rukwama kukuu za wazegaz...