Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2012

SIRI ZA 'JAM' JIJINI NAIROBI

MTUNZI:ODHIAMBO DANYELL Dereva wa basi la kampuni ya RWAKEN alijistiri mbele ya usukani na kupiga gari moto wakati tukiondoka katika kitivo cha chuo kikuu cha Daystar yenye makao katika mzunguko wa barabara ya Valley road, Nairobi. Il ikuwa dakika chache baada ya saa kumi na nusu jioni. Hii ni kumaanisha, wafanyikazi pamoja na wanafunzi wa mchana chuoni tayari walikuwa katika harakati zakufunganya virago na kurejea makwao baada ya panda shuka za mchana. Vvrrrrrrrrrrrrrm! vvrrrrrrrm! Dereva alipasha gari moto na taratibu basi likaelekezwa nje ya lango kuu. kabla ya kuingia kwenye barabara kuu ya Valley road. Auuuuuwi! imagine mbele yetu palisimama gari aina ya Range Rover Vogue iliyowachilia moshi nyeupe iliyosokota na kupata hifadhi katika mapua ya basi la RWAKEN. Katika mbuga la wanyama, gari hili linalinganishwa na mfalme Simba kutokana na udhabiti wake. Mashini hii yasifika kwa ulafi wa petroli pamoja na muundo wake wa kutamanisha. Aha! Sasa nimejua kwanini basi ilikuw...

USHUHUDA WA MKIMBIZI

Januari tarehe 23, 2012 Saa iliyotulia wima kwenye kuta ya hema ilifichua kwamba ilibakia dakika chache kabla ya saa nane mchana . Akilini halikunijia wazo kwamba jaji wa mahakama ya Hague Bi Ekaterina Trendafilova alikuwa anasubiriwa kutoa uamuzi wa korti dhidi ya washukiwa sita wa vita vya baada ya uchaguzi. Msimu wa masika tayari ulikuwa umeenda likizo, kiangazi kilikuwa kinatawala na umaarufu wa jua kijijini ungedhihirika kwa jinsi miale yake ilizidi kukausha nchi kavu hata nyufa zikatawala ardhini.  kambi ya wakimbizi ya faraja Mara kwa mara, tufani kali za kutoka magharibi zingesikika zikifagilia na kufanya matawi ya miembe kupukutika kabla ya kuchezeshwa angani ovyo ovyo. Nilikuwa nimetulia kwenye mkeka ndani ya hema ndipo nikagutushwa na unyamale uliojiri kwenye kambi ya wakimbizi ya faraja. Mara moja, nikashuku hatari na kuchungulia nje angalau kuhakikisha kila kitu kilikuwa sawa. Nikisimama kwenye mlango ya hema, ningehisi hali isiyo ya kawaida. Upweke ulitawala k...