MTUNZI:ODHIAMBO DANYELL Dereva wa basi la kampuni ya RWAKEN alijistiri mbele ya usukani na kupiga gari moto wakati tukiondoka katika kitivo cha chuo kikuu cha Daystar yenye makao katika mzunguko wa barabara ya Valley road, Nairobi. Il ikuwa dakika chache baada ya saa kumi na nusu jioni. Hii ni kumaanisha, wafanyikazi pamoja na wanafunzi wa mchana chuoni tayari walikuwa katika harakati zakufunganya virago na kurejea makwao baada ya panda shuka za mchana. Vvrrrrrrrrrrrrrm! vvrrrrrrrm! Dereva alipasha gari moto na taratibu basi likaelekezwa nje ya lango kuu. kabla ya kuingia kwenye barabara kuu ya Valley road. Auuuuuwi! imagine mbele yetu palisimama gari aina ya Range Rover Vogue iliyowachilia moshi nyeupe iliyosokota na kupata hifadhi katika mapua ya basi la RWAKEN. Katika mbuga la wanyama, gari hili linalinganishwa na mfalme Simba kutokana na udhabiti wake. Mashini hii yasifika kwa ulafi wa petroli pamoja na muundo wake wa kutamanisha. Aha! Sasa nimejua kwanini basi ilikuw...
JAMVI LA BURUDANI,MAARIFA NA USHAURI