Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2011

FEDHEHA ZA SWALEH

MTUNZI: MARIA REHEMA Swaleh kijana wa miaka ishirini na tisa alienda usingizini, akiwaza na kuwazua jinsi atakavyo jishindia jiko. Alihesabu miaka yake na kustaajabu kuwa miaka hiyo yote, alikuwa anavunda upweke. Kisa na maana hakuwa na bila barafu wa roho. Liwike lisiwike kutakucha. Swaleh aliamka na kabla ya kupata staftahi, alianza siku kwa kujipodoa. Liche ya uzito wake na kipipa cha tumbo, aliamua kuvaa shati na suruale iliyombana kupindukia. “ Ndo mavazi ya kisasa haya, nitaweza kuwapata warembo kadhaa,” alijiambia Swaleh. Baada ya staftahi, Swaleh huyo kiguu na njia jijini kutafuta kipenzi cha roho. Bak bandika bak bandua mpaka kwenye kituo cha basi. Alipoingia kwenye ‘matatu’ moja akakutana na kidosho aliyerembeka mno. Hakupoteza wakati alikimbia na kuketi karibu na mrembo huyo. Alivutiwa na macho yake makubwa yaliyong’aa na ngozi yake nyororo. Mwili wake je? Nikisema zaidi utamwonea wivu. Maumbile haya yalimtia Swaleh wazimu. Bila shaka Swaleh alibaki md...

NIMESADIKI MOMBASA NI KITOVU CHA STAREHE.

Na Odhiambo Danyell Mawingu mepesi yalitawanyika angani utadhani yameanikwa ili kukaushwa na miale ya jua ambayo yalikuwa yanazidi kufifia. Ghafla ,upepo mkali ulifagilia kwenye nchi kavu na kuwacha matawi ya miti yakipukutika ovyo ovyo kabla ya kuchezeshwa angani. Isitoshe, ilihamisha wingu moja baada ya nyingine hata anga ikabaki safi. Kilichobaki kuonekana ni kundi ndogo la kunguru