Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2012

KIVULI KIZITO CHA KIWEWE

MTUNZI: ODHIAMBO DANYELL Wa kwanza alikuwa Rehema, njia zetu zilikutana kwenye ufuo wa bahari hindi msimu wa upanzi wa mwaka 1999. Kidonda hicho kingali kibichi. Japo nilibaki na kovu, nahisi ni kama nazungumzia ya jana. Kwa ufupi, yake na yangu yalikuwa mafupi hata ingawa vioja vilikuwa teletele. Uhusiano wa kunoga tulilinda kwa takriban miezi miwili. Siku moja, aliamka na kuniambia yu mja mzito. Nilimshauri akakiangamize kijusi hicho. Hii ilitokana na wingi wa uoga kuhusu majukumu ambayo yangendamana na hali hiyo. Alikubali wito japo shingo upande. Baadaye, niliarifiwa yuko hali mahututi katika katika zahanati ya Dr. Tiba wa Maradhi. Kesho yake Jioni , nilipata simu ya dharura. “harakisha mpenzio amevuja damu nyingi sana akijaribu kuavya mimba changa. Nasikitika kusema, si wa dunia hii tena.” hitimisho likawa ni maombolezi na baadaye mazishi huku vidole zote nikielekezewa. Vivyo hivyo, aliyefuatilia mkondo huu alikuwa kipusa kwa jina Amina. Mtoto yatima ambaye nilipata kum...